Marekani kuiwekea vikwazo Syria:
7 Machi 2004Matangazo
WASHINGTON:
Marekani imo njiani kuiwekea Syria vikwazo vya
kiuchumi na kisiasa kwa sababu ya kuunga mkono
kwake makundi ya kigaidi, aliarifu mtumishi wa
Rais George W. Bush. Nao wabunge wa Kimarekani
walithibitisha taarifa hiyo kabla ya kutangazwa
kwake rasmi. Hapo mwezi wa Novemba bunge la
Marekani liliunga mkono kimsingi kuwa Syria
iwekewe vikwazo vya kiuchumi na kisiasa.
