UchumiMarekani
Marekani na China zafanya mazungumzo ya kibiashara
15 Machi 2026
Matangazo
Ujumbe wa Marekani unaongozwa na Waziri wa Fedha Scott Bessent, huku China ikiwakilishwa na Naibu Waziri Mkuu He Lifeng. Pande hizo mbili zinajadili masuala ya pamoja ya biashara na uchumi.
Ziara ya Trump itakuwa ya kwanza ya rais wa Marekani nchini China tangu mwaka 2017, wakati alipoizuru nchi hiyo kwenye muhula wake wa kwanza. Na inakuja miezi michache baada ya Trump na Xi Jinping kukubaliana kusitisha kwa muda mgogoro wa kibiashara uliosababisha ushuru mkubwa kati ya mataifa hayo mawili.
Hata hivyo, mvutano wa kibiashara bado upo. Mazungumzo hayo pia yanaweza kugusia vita vya Iran na athari zake kwa bei na usambazaji wa mafuta duniani.