1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Marekani na Denmark kukutana kujadiliana suala la Greenland

14 Januari 2026

Waziri wa Mambo ya Nje wa Denmark Lars Løkke Rasmussen atakutana Jumatan mjini Washington na Makamu wa Rais wa Marekani JD Vance na Waziri wa Mambo ya Nje Marco Rubio kuangazia suala la Greenland.

Greenland Nuuk 2026 | Wakazi na wanasiasa wa Greenland wakataa pendekezo la Donald Trump la kukiweka kisiwa hicho chini ya mamlaka ya Marekani
Wakazi na wanasiasa wa Greenland wakataa pendekezo la Donald Trump la kukiweka kisiwa hicho chini ya mamlaka ya MarekaniPicha: Lokman Vural Elibol/Anadolu Agency/IMAGO

Waziri wa Mambo ya Nje wa Denmark Vivian Motzfeldt pia atahudhuria kikao hicho.

Mkutano huo ulikuwa umekubaliwa katika ngazi ya mawaziri wa mambo ya nje na kulingana na Waziri Mkuu wa Denmark Mette Frederikssen, Vance alifanya maamuzi ya dakika za mwisho kuhudhuria kikao hicho.

Frederiksen na Waziri Mkuu wa Greenland Jens-Frederik Nielsen walisisitiza jana Jumanne mbele ya waandishi wa habari huko Copenhagen kwamba Greenland haiuzwi na haiwezi kuunganishwa na Marekani.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW