Marekani, washirika wapendekeza mpango kusitisha vita Sudan
13 Septemba 2025
Nchi hizo zimependekeza pia lengo la usitishaji vita wa kudumu utakaofuatiwa na uongozi wa mpito kwa miezi tisa kuelekea utawala wa kiraia. Katika taarifa ya pamoja iliyotolewa na Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani, nchi hizo nne chini ya mwamvuli wao unaojulikana kama Quad, zimesema kipindi cha mpito kinapaswa kukidhi matarajio ya watu wa Sudan kuelekea kuanzishwa kwa urahisi serikali huru, itakayoongozwa kiraia na yenye uhalali mpana na uwajibikaji.
Sudan imekuwa katika vita vya umwagaji damu vya kugombea madaraka tangu mwezi Aprili mwaka 2023 kati ya kiongozi wa kijeshi Abdel-Fattah al-Burhan na makamu wake wa zamani Abdel-Fattah al-Burhananayeongoza vikosi vya RSF.Umoja wa Mataifa umesema machafuko hayo yamesababisha mgogoro mbaya wa kibinadamu ukosefu mkubwa wa chakula wakati maelfu ya watu wamekufa na wengine mamilioni wamelazimika kuyahama makazi yao.