1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroMamlaka ya Palestina

Marekani: Netanyahu apaswa kuwadhibiti walowezi

30 Oktoba 2023

Mshauri wa rais wa Marekani kuhusu usalama wa taifa, Jake Sullivan amesema Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu anapaswa kuwadhibiti walowezi wenye misimamo mikali katika Ukingo wa Magharibi.

USA | Jake Sullivan Nationaler Sicherheitsberater
Mshauri wa rais wa Marekani kuhusu usalama wa taifa, Jake SullivanPicha: Susan Walsh/AP Photo/picture alliance

Marekani imemtaka pia Netanyahu kuwawajibisha kwa mashambulizi wanayoyafanya dhidi ya Wapalestina.  Awali, Rais wa Marekani Joe Biden, amewatuhumu walowezi hao wa kiyahudi kwa alichokiita ''kumwaga mafuta kwenye moto'' kwa ghasia zinazofanyika katika Ukingo wa Magharibi, wakati Israel ikilipiga vita kundi la Hamas katika Ukanda wa Gaza.

Soma pia: Guterres aonya Gaza inaendelea kuteseka 'kila baada ya saa'

Wakati huo huo, Waziri Mkuu wa Uingereza Rishi Sunak na Rais Emannuel Macron wa Ufaransa wamezungumza jana, na kuahidi kuwa nchi zao zitashirikiana katika kuhakikisha kuwa msaada wa chakula, maji, madawa na mafuta unawafikia wanaouhitaji katika Ukanda wa Gaza.

Kwa mujibu wa wizara ya Afya huko Gaza inayodhibitiwa na Hamas, zaidi ya Wapalestina 8,000 wameuawa tangu kuanza kwa vita hivyo Oktoba 7 mwaka huu.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW