SiasaMarekani
Marekani yaadhimisha miaka 250 ya Uhuru wake
4 Julai 2026
Matangazo
Akizungumza mbele ya wafuasi wake kwenye eneo la Kumbukumbu ya Kitaifa ya Mlima Rushmore eneo takatifu lililotengwa kwa ajili ya kuwakilisha msingi, maendeleo na Demokrasia ya Marekani katika jimbo la South Dakota,Trump amesema mtu anaweza kuchagua kati ya kuwa mkomunisti ama mzalendo.
Katika siku za hivi karibuni, Trump amekuwa akilitumia neno "ukomunisti" kuwakosoa wapinzani wake wa kisiasa wa mrengo wa kushoto na sera zao.
Trump pia ameielezea Marekani kama taifa linalomtegemea Mungu, akisema haki zao wamepewa na Mungu aliyewaumba, na hazitakiwi kuvunjwa.
Rais huyo mwenye umri wa miaka 80 pia amesema hakuna nchi nyingine iliyoitendea mema zaidi dunia kuliko Marekani.