Marekani yaahidi kusimama na washirika wa NATO
23 Septemba 2025
Matangazo
Balozi wa Marekani katika Umoja wa Mataifa, Mike Waltz ameuambia mkutano wa dharura wa Baraza la Usalama la umoja huo mjini New York kwamba Marekani inasimama na washirika wake wa NATO katika kukabiliana na ukiukaji huo wa anga.
Waltz amesena Urusi inapaswa kuwacha mara moja tabia yake hiyo hatari, kwani inasababisha kitisho kwa usalama wa Ulaya.
Siku ya Ijumaa, Estonia iliripoti kwamba ndege tatu za kivita za Urusi ziliingia katika anga yake kwa dakika 12.
Hata hivyo, Urusi imekanusha kuhusika na ukiukaji huo.
Aidha, droni kadhaa za Urusi ziliingia katika anga ya Poland wiki moja kabla, wakati wa shambulizi la anga la Urusi nchini Ukraine.