1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Marekani yaanza tena kutoa msaada wa chakula Ethiopia

15 Novemba 2023

Shirika la Marekani la Maendeleo ya Kimataifa - USAID litaanza tena kutoa misaada ya chakula nchini Ethiopia Desemba mwaka huu.

Symbolbild I Hunger in der Welt noch groß
Picha: Ben Curtis/AP/picture alliance

Tangazo hilo limejiri ikiwa ni miezi mitano baada ya kusitisha mpango wake wa kitaifa kutokana na ufisadi mkubwa uliofanywa na maafisa wa nchini Ethiopia.

Msemaji wa USAID Jessica Jennings amesema kurejeshwa kwa shughuli hizo za misaada kumetokana na mageuzi mapya yaliyofanywa na shirika hilo ili kuimarisha usajili wa wanufaika na ufuatiliaji wa nafaka zinazotolewa.

Jeshi la Ethiopia larejesha udhibiti mji wa Lalibela

Amesema hatua hizo mpya zitajaribiwa kwa mwaka mmoja, akiongeza kuwa zitabadilisha pakubwa mfumo wa msaada wa chakula nchini Ethiopia na kusaidia kuhakikisha kuwa msaada unawafikia wanaokumbwa na uhaba mkubwa wa chakula.

Mwezi uliopita USAID ilianza tena kutoa msaada wa chakula kwa wakimbizi milioni moja baada ya serikali ya Ethiopia kukubali kujiondoa katika shughuli za utolewaji, uhifadhi na usambazaji wa msaada wa chakula cha wakimbizi.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW