1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Marekani yailaumu Rwanda kwa kuhatarisha usalama

13 Desemba 2025

Marekani imeilaumu Rwanda kwa kuchochea vita vya kikanda kwa kuunga mkono waasi wa M23 mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, siku chache tu baada ya kusainiwa kwa mkataba wa amani uliosimamiwa na Marekani.

Marekani, New York 2025 | Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa
Balozi wa Marekani katika Umoja wa Mataifa, Mike WaltzPicha: Adam Gray/AFP/Getty Images

Balozi wa Marekani katika Umoja wa Mataifa Mike Waltz, jana Ijumaa aliliambia Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kwamba badala ya kupiga hatua kuelekea amani kama walivyoona chini ya uongozi wa Rais Donald Trump katika wiki za hivi karibuni, Rwanda inaongoza eneo hilo kuelekea ukosefu wa utulivu na vita.

Pia amesema Marekani ina wasiwasi mkubwa na inazidi kukatishwa tamaa kwa kuzuka upya kwa ghasia.

Waltz ameongeza kuwa vikosi vya ulinzi vya Rwanda vimetoa msaada wa vifaa, mipangilio na mafunzo kwa M23 pamoja na kuisadia vitani nchini Kongo kwa kupeleka takriban wanajeshi 5,000 hadi 7,000, bila kujumuisha uwezekano wa nyongeza ya idadi hiyo wakati wa mashambulizi ya hivi karibuni.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW