1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Marekani yaiondolea Belarus baadhi ya vikwazo vya kibiashara

13 Desemba 2025

Marekani imesema inaondoa baadhi ya vikwazo vya kibiashara dhidi ya Belarus katika ishara ya hivi karibuni ya maelewano kati ya Washington na nchi hiyo iliyotengwa.

Urusi Moscow 2023 | Alexander Lukaschenko
Rais wa Belarus Alexander Lukaschenko akiwasili katika ikulu ya Kremlin mnamo Mei 25, 2023Picha: Ilya Pitalev/TASS/dpa/picture alliance

John Coale, mjumbe maalum wa Marekani kwa Belarus, alitangaza hilo baada ya kukutana na kiongozi wa Belarus Alexander Lukashenko mjini Minsk jana na leo.

Akizungumza na waandishi wa habari leo, Coale aliyataja mazungumzo ya siku hiyo mbili kuwa yenye tija.

Mjumbe huyo wa Marekani amesema kurejesha uhusiano wa kawaida kati ya Washington na

Minsk lilikuwa lengo lao.

Kwa mujibu wa shirika la habari la Belarus Belta, Coale amesema wanaondoa vikwazo, wanawaaachilia wafungwa, wanaendelea na mazungumzo na kwamba uhusiano kati ya nchi hizo ulikuwa unatoka kuwa mchanga hadi kwa hatua ya kujiamini zaidi.

Kwa upande wake Rais Lukashenko amewasamehe wafungwa 123 kwa kubadilshana na na kuondolewa kwa vikwazo hivyo vya Marekani.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW