MigogoroAfrika
Marekani yaiwekea vikwazo Rwanda kwa kuwaunga mkono M23
3 Machi 2026
Matangazo
Tangazo la vikwazo hivyo limetolewa jana jioni na Wizara ya Fedha ya Marekani ambayo imedai kwamba bila msaada wa serikali na jeshi la Rwanda, kundi la M23 lisingeweza kufanya mashambulizi nchini Kongo. Kwa miaka mingi sasa inaaminika kuwa Rwanda ndiye mfadhili mkuu wa kundi la M23
Miongoni mwa waliowekewa vikwazo ni Mkuu wa Jeshi la Rwanda, Jenerali Mubarakh Muganga, Mnadhimu Mkuu wa Jeshi, Vincent Nyakarundi na makamanda wengine wawili wa ngazi ya juu.
Utawala wa Rais Donald Trump umekasirishwa na kuendelea kwa mashambulizi ya kundi la M23 licha ya kutiwa saini kwa makubaliano ya amani kati ya Marais Felix Tshisekedi wa Kongo na Paul Kagame wa Rwanda mjini Washington Disemba mwaka jana.