Migogoro
Marekani yaliwekea vikwazo jeshi la Rwanda kutokana na mzozo
3 Machi 2026
Matangazo
Taarifa iliyotolewa na Wizara ya fedha ya Marekani imefafanua kuwa watuhumiwa waliwasaidia waasi hao kupata udhibiti wa ardhi ikiwemo migodi muhimu mashariki mwa Kongo.
Matumaini ya kupata amani mashariki mwa Kongo yanazidi kufifia
Vikwazo hivyo vimetangazwa licha ya makubaliano ya amani yaliyosainiwa kati ya Rwanda na Kongo yaliyosimamiwa na Marekani. Lakini hata baada ya makubaliano hayo, waasi wa M23 waliuteka mji wa Uvirana bado wanaendelea na operesheni zao katika eneo la mpaka na Burundi.
Serikali ya Rwanda imeikosoa hatua ya Marekani ya kuiwekea vikwazo ikisema taifa hilo kubwa limeegemea upande mmoja, huku ikiilaumu Kongo kwa kushindwa kutekeleza makubaliano yanayolenga kuutatua mzozo huo.