1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Marekani yataka kumhamishia Liberia raia wa Salvador

25 Oktoba 2025

Serikali ya Marekani imesema inataka kumhamishia nchini Liberia raia wa Salvador Kilmar Abrego Garcia kufikia mwishoni mwa mwezi huu. Hatua hizo imekuja katikati mwa mzozo kuhusu mpango wa uhamiaji wa Rais Donald Trump .

USA Tennessee 2025 | Kilmar Abrego Garcia
Kilmar Abrego Garcia anayetarajiwa kuhamishwa na Marekani hadi LiberiaPicha: Seth Herald/REUTERS

Katika ombi lililowasilishwa katika mahakama ya Maryland jana Ijumaa, mawakili wa serikali walisema wameichagua Liberia kama eneo la kumhamishia mhamiaji huyo kwa sababu haikuwa katika orodha ya nchi ambazo mawakili wa Abrego Garcia walikuwa wameikataa.

Mawakili hao wamesema Liberia ni taifa lenye demokrasia iliyostawi na mojawapo ya washirika wa karibu wa Marekani katika bara la Afrika.

Serikali pia imebainisha kuwa Liberia ni nchi inayozungumza Kiingereza na imejitolea kuwachukulia wakimbizi kibinadamu.

Mawakili wa Abrego Garcia hawakujibu mara moja ombi la tamko kuhusu hali hiyo.

Kesi ya Abrego Garcia, ambaye mwezi Machi alihamishiwa kimakosa hadi El Salvador na kisha kurejeshwa Marekani mwezi Juni, imewavutia wengi wanaopinga juhudi za Trump za kuwahamisha wahamiaji wengi kutoka Marekani.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW