1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Marekani yatiwa wasiwasi na mashambulizi ya RSF

Hawa Bihoga
19 Oktoba 2023

Marekani inasema ina wasiwasi mkubwa kutokana na ripoti kwamba kikosi cha wapiganaji wa RSF nchini Sudan wamezidisha mashambulizi katika mkoa ya Darfur na mji mkubwa wa Omdurman.

Sudan | Mohamed Hamdan Daglo
Kiongozi wa kundi la RSF nchini Sudan, Mohamed Hamdan Daglo.Picha: Ashraf Shazly/AFP

Msemaji wa wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani Matthew Miller, amesema nchi hiyo ina wasiwasi mkubwa kutokana na ripoti kwamba kikosi cha wapiganaji cha RSF nchini Sudan wamezidishisha mashambulizi katika mikoa ya Darfur Kusini na Omdurman.

Soma zaidi: UN: Miezi sita ya mapigano nchini Sudan yasababisha vifo vya takriban watu 9,000

Mapigano kati ya Jeshi la Sudan na RSF yalizuka Aprili 15 kufuatia mzozo unaohusiana na mpango wa mpito kuelekea utawala wa kiraia, na yameuharibu mji mkuu wa Khaeroum na kusababisha mashambulizi yanayochochewa na ukabila katika eneo la Darfur. 

Miller amesema Marekani imeitolea wito RSF kuacha mara kushambulia maeneo ya raia, na kuwalinda raia.
 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW