1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Marekani yatowa dola $5M kumpata kiongozi wa al-Shabaab

18 Oktoba 2023

Marekani imetoa ahadi ya zawadi ya dola milioni 5 kwa taarifa kuhusu kiongozi wa kundi la Al Shabaab nchini Somalia, Abukar Ali Adan.

Al-Schabaab Miliz in Somalia
Baadhi ya wapiganaji wa kundi la al-Shabaab waliokamatwa na vikosi vya Umoja wa Mataifa nchini Somalia.Picha: Tobin Jones/Au Un Ist/dpa/picture alliance

Wizara ya mambo ya nje ya Marekani imesema Abukar Ali Adan, ambaye alitangazwa rasmi kama gaidi na Marekani mnamo 2018, ni naibu kamanda wa al-Shabaab na anahusishwa na matawi kadhaa ya mtandao wa kigaidi ya al-Qaida.

Wizara hiyo pia imesema kundi la Al Shabaab linaendelea kupanga na kufanya njama za vitendo vya kigaidi dhidi ya Marekani, maslahi ya Marekani na washirika wake wa kigeni.

Soma zaidi: Watu 35 wauawa kwenye mapigano kati ya jeshi na Al Shabaab

Wakati huo huo, Waziri wa Mambo ya Ndani wa Kenya Kithure Kindiki ameapa vita kamili dhidi ya al-Shabaab na kutaja watu 35 wanaoshukiwa kuwa wanachama wa kundi hilo na waliohusika na mashambulizi katika mpaka wa nchi hiyo na Somalia.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW