1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Marekani yatuma ndege za misaada ya kibinadamu Gaza

28 Novemba 2023

Marekani leo imepeleka ndege tatu za kijeshi nchini Misri ambazo zitafikisha misaada muhimu ya kibinadamu katika ukanda wa Gaza baada ya makubaliano ya kusitisha mapigano kati ya Israel na kundi la Hamas.

Rais wa Marekani Joe Biden
Rais wa Marekani Joe BidenPicha: Stephanie Scarbrough/AP/picture alliance

Ndege hizo za kijeshi zilizobeba vyakula, vifaa vya matibabu na nguo nzito za majira ya baridi, ni msaada wa kwanza kutolewa na jeshi la Marekani tangu kuanza kwa mzozo kati ya Israel na Hamas Oktoba 7.

Msaada huo umetokea siku moja tu baada ya Rais Joe Biden kueleza kuwa, atatumia mwanya wa usitishwaji wa mapigano kupeleka misaada zaidi Gaza.

Soma pia:Mzozo wa Israel-Hamas: Mateka zaidi watarajiwa kuachiwa

Umoja wa Mataifa utauchukua msaadahuo wa Marekani kutoka eneo la Sinai kaskazini mwa Misri unaopakana na ukanda wa Gaza unaotawaliwana Hamas, na kuusafirisha hadi ndani ya mamlaka ya Palestine.

Ndege nyengine mbili za Marekani zilizobeba msaada zaidi zinatarajiwa kuwasili katika siku chache zijazo.
 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW