1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mashambulio ya Israel na Iran yaendelea kutikisa

9 Machi 2026

Israel imefyetuwa makombora zaidi kuelekea Iran na Lebanon, huku Iran ikishambulia mataifa ya Ghuba na Israel kujibu

Moshi mzito umetanda kwenye anga la mji mkuu Tehran baada ya depo ya mafuta kushambuliwa na makombora ya Israel na Marekani
Moshi mzito umetanda kwenye anga la mji mkuu Tehran baada ya depo ya mafuta kushambuliwa na makombora ya Israel na MarekaniPicha: Sasan/Middle East Images/SIPA/picture alliance

Israel imeendelea na operesheni za kijeshi dhidi ya maeneo kadhaa nchini Iran na Lebanon leo Jumatatu.

Jeshi la nchi hiyo limefahamisha kupitia taarifa kwenye mtandao wa Telegram, kwamba wimbi la mashambulizi ya anga yamefanywa dhidi ya miundo mbinu ya utawala wa Iran, na kundi lenye mafungamano na utawala huo la Hezbollah mjini Beirut.

Iran yaingia enzi mpya ya uongozi wa Mojtaba huku vita ikienea

Iran pia imefanya mashambulio mengine zaidi dhidi ya Israel na mataifa ya Ghuba leo Jumatatu saa kadhaa zikiwa zimepita baada ya kumtangaza Mojtaba Khamenei kuwa kiongozi wa juu anayerithi nafasi ya babake aliyeuliwa na Marekani, Ayatollah Ali Khamenei.

Kufuatia mashambulio hayo yaliyolenga pia kinu cha mafuta cha Saudi Arabia cha Shaybah, Riyadh  imeionya Iran kwa maneno makali, ikisema nchi hiyo itashindwa vibaya ikiwa itaendelea kuyashambulia mataifa ya kiarabu.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW