1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mashambulizi ya bomu yaua watu 6 Nigeria

Martin,Prema/dpa17 Juni 2011

Watu 6 wameuawa katika mashambulizi mawili ya bomu siku ya Alkhamisi nchini Nigeria.

Katika shambulizi moja la kujitoa mhanga, bomu liliripuliwa katika gari mbele ya makao makuu ya polisi katika mji mkuu Abuja. Watu 2 waliuawa katika shambulio hilo na lilisababisha magari kadhaa kushika moto.

Saa chache baadae, bomu jingine liliripuka karibu ya kanisa katika mji wa Damboa ulio katika jimbo la Borno kaskazini-mashariki ya Nigeria. Kwa mujibu wa polisi, vijana 4 waliuawa na mtu mmoja alijeruhiwa.

Kundi la madhehebu ya Boko Haram lenye itikadi kali za Kiislamu limedai kuwa ndio lililohusika na shambulio la Abuja.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW