1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mashambulizi ya Urusi Ukraine yawajeruhi sita mjini Odesa

31 Desemba 2025

Jeshi la Ukraine limesema mashambulizi ya Urusi yamewajeruhi watu sita mjini Odesa wakiwemo watoto watatu wa miaka minane, 14 na miezi 7.

Ukraine: Gebäude in Flammen nach russischem Angriff auf Odessa
Mashambulizi ya Urusi Ukraine yawajeruhi sita mjini Odesa Picha: Emergency Service Ukraine / AFP

Kiongozi wa Jeshi mjini humo  Oleg Kiper, amesema mashambulizi hayo ya droni yalivurumishwa kuilenga miundumbionu  ya nishati, na makaazi ya watu.

Taarifa zaidi zinasema mwanamume wa miaka 42 pia alijeruhiwa na yuko katika hali mbaya hospitalini. Kwa sasa sehemu ya mji huo haina umeme pamoja na maji. Kwengineko mashambulizi mengine ya droni kutoka Urusi yaliwajeruhiu watu wawili katika jimbo la Dnipropetrovsk.

Mashambulizi haya yanajiri baada ya Ukraine kukanusha kushambulia makazi ya Rais wa Urusi Vladimir Putin na kuituhumu Moscow kusema uwongo ili kusambaratisha mazungumzo ya kusitisha vita Ukraine. Moscow imesema kitendo ilichofanyiwa nchi yake ni cha kigaidi.

Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky, aliyesema madai ya Urusi ni ya kupanga, atakutana na washirika wake Januari 6 nchini Ufaransa katika juhudi za kuendeleza juhudi za kusaka amani.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW