1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroUlaya

Mashambulizi ya Urusi yasababisha maafa Ukraine

24 Januari 2026

Mashambulizi ya Urusi dhidi ya Ukraine yamesababisha kifo cha mtu mmoja na kujeruhiwa kwa wengine 23 usiku wa kuamkia leo.

Ukraine Kyiv 2026 | Athari za mashambulizi ya Urusi nchini Ukraine
Athari za mashambulizi ya Urusi nchini Ukraine.Picha: Valentyn Ogirenko/REUTERS

Maafa hayo yametokea katika wakati ambapo wajumbe wanaoshiriki mazungumzo ya amani kutoka Ukraine, Urusi na Marekani wakitarajiwa kukutana Abu Dhabi leo kwa siku ya pili ya mazungumzo ya kumaliza uvamizi huo wa Urusi wa takriban miaka minne.

Kulingana na kiongozi wa jeshi mjini Kyiv Tymur Tkachenko, mtu huyo mmoja aliuawa na wengine wanne wamejeruhiwa katika shambulizi la droni la Urusi kwenye mji mkuu Kyiv.

Wengine 19 wamejeruhiwa kwenye mji wa pili kwa ukubwa nchini Ukraine wa Kharkiv. Hayo yameelezwa na Meya wa mji huo Ihor Terekhov.

Mazungumzo ya wajumbe hao wa mataifa hayo matatu, ni tukio la kwanza linalojulikana ambapo maafisa wa utawala wa Marekani wamekaa na nchi zote mbili Ukraine na Urusi kama sehemu ya msukumo wa Washington wa kutaka kumaliza uvamizi huo wa Urusi nchini Ukraine.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW