Mashirika yataka Diallo aachiwe huru
4 Desemba 2023
Matangazo
Muungano wa mashirika hayo umesema Diallo alitekwa nyara siku ya Ijumaa (Disemba 1) na watu waliovalia nguo za kiraia nje ya ofisi za serikali mjini Ouagadougou.
Mashirika hayo yameeleza kuwa hakujatolewa taarifa zozote za Diallo au maelezo juu ya sababu za kutekwa kwake na yametoa wito wa kuachiliwa pamoja na kuhakikisha usalama wake.
Soma zaidi: Mali, Niger na Burkina Faso zakusudua kuunda shirikisho
Kwa mujibu wa shirika la Human Rights Watch, Diallo ambaye ni mshindi wa tuzo ya Martin Ennals mnamo mwaka 2022 inayotolewa kwa watetezi wa haki za binaadamu, alikuwa mmoja kati ya wakosoaji wakuu wa serikali ya Burkina Faso ambaye hivi karibuni, alitakiwa kujiunga na jeshi la nchi hiyo katika vita dhidi ya wapiganaji wa itikadi kali.