Allegri aihama Juventus
20 Mei 2019Matangazo
Lakini wanampoteza kocha wao Massimiliano Allegri ambaye anaondoka baada ya kuhudumu kama mkufunzi kwa kipindi cha miaka mitano.
Allegri mwenye umri wa miaka hamsini na moja anasema lakini kuwa anaondoka ila hana kinyongo na yeyote.
"Tumezungumza na wakuu wa klabu na tukaelezana kile kilicho bora kwa Juventus na mustakabali wake. Baada ya hapo wakuu wakaitathmini hali nzima na ikaamuliwa ni vyema kwamba nisiwe kocha wa klabu hii msimu ujao. Hili halibadilishi chochote kwasababu hali ya maelewani na Rais Agnelli, wakurugenzi Pavel Nedved na Fabio paratici bado yanasalia kuwa mazuri kabisa," alisema Allgeri.