Mataifa ya Bahari ya Kaskazini kukuza nishati ya upepo
26 Januari 2026
Mataifa tisa ya Ulaya yamekubaliana leo kukuza uzalishaji wa nishati ya upepo katika Bahari ya Kaskazini, kwa lengo la kuongeza nishati safi kwa mazingira na kupunguza utegemezi wa Urusi na mataifa mengine ya kigeni.
Makubaliano hayo yamefikiwa leo katika mkutano wa tatu wa nchi zinazopakana na Bahari ya Kaskazini unaofanyika Hamburg, Ujerumani. Waziri wa uchumi na nishati wa Ujerumani Katherina Reiche amesema kuwa.
"Lengo letu ni kuendeleza hifadhi kubwa zaidi ya nishati duniani, na manufaa ya upanuzi huu yako wazi: tunaongeza usalama wa upatikanaji wa nishati, tunaimarisha sekta yetu ya baharini, tunaongeza thamani ya kiuchumi, na ajira bora zenye viwango vya juu"
Ujerumani, Ufaransa, Uingereza na Denmark ni miongoni mwa nchi zilizotia saini makubaliano ya kuifanya Bahari ya Kaskazini kuwa hifadhi kubwa zaidi ya nishati safi duniani.