1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaUrusi

Mataifa ya Magharibi; Urusi iwajibishwe kwa uvamizi Ukraine

3 Aprili 2024

Kongamano la uhalifu wa kivita la kundi la mataifa 44 ya Magharibi lililofanyika mjini the Hague nchini Uholanzi, limesema kuwa lazima Urusi ilipie uharibifu iliosababisha nchini Ukraine

Maafisa wa zima moto wakabiliana na moto uliozuka baada ya shambulizi la kombora la Urusi mjini Odesa nchini Ukraine mnamo Desemba 29,2023
Maafisa wa zima moto wakabiliana na moto uliozuka baada ya shambulizi la Urusi mjini Odesa, UkrainePicha: Oleksandr Gimanov/AFP

Katika tamko lililotolewa mwishoni mwa kongamano hilo la uhalifu wa kivita, mataifa hayo yalisema kuwa Urusi inapaswa kufunguliwa mashitaka kwa vita vyake vya uchokozi na kuwajibikia matendo yake.

Walioshiriki kongamano la uhalifu wa kivita 

Kongamano hilo lilijumuisha mawaziri na waakilishi wa Halmashauri kuu ya Umoja wa Ulaya pamoja na mahakama za kimataifa walioalikwa naUkrainena Uholanzi kujadili kuhusu uwezekano wa kufungua kesi ya uhalifu wa kivita unaodaiwa kufanyika nchini Ukraine.

Soma pia:Ukraine yakabiliwa na matatizo ya umeme kufuatia mashambulizi ya Urusi

Waakilishi wa mataifa yasiokuwa ya Ulaya kama vile Marekani , Canada na Australia pia walihudhuria.

Washiriki wa kongamano hilo, walisema kuwa wamejitolea kuhakikisha kuundwa kwa jopo maalumu la kuchunguza na kushitaki uhalifu uliofanywa na Urusi nchini Ukraine.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW