Wakaazi wa Florida huko Marekani watakusanyika leo kuwaomboleza watu 17 waliouwawa na mtu mmoja aliyekuwa amejihami kwa bunduki katika shule moja mjini humo. Maafisa wa usalama kwa sasa bado wanachunguza jinsi mwanamume huyo mwenye umri wa miaka 19 aliyekuwa mwanafunzi wa zamani wa shule hiyo Nikolas Cruz alivyopenya na kuwashambulia wanafunzi na walimu.