Mauaji ya ''El Mencho'' yazusha taharuki Mexico
23 Februari 2026
Hali ya wasiwasi imeongezeka nchini Mexico,shule zimefungwa katika majimbo mengi ya nchi hiyo wakati serikali na mataifa ya kigeni wakitowa tahadhari kwa raia wao kubakia majumbani.
Wasiwasi huo umesababishwa na machafuko yaliyozuka kufuatia kuuwawa kwa kiongozi wa mtandao wenye nguvu wa uhalifu unaofahamika kama ''Jalisco New Generation''.
Nemesio Ruben Osequera Cervantes kwa jina maarufu ''El Mencho'' aliyeuwawa na wanajeshi alikuwa kiongozi wa kundi hilo linalotajwa kukuwa kwa kasi na ambalo limekuwa likihusika na kupeleka mihadarati nchini Marekani.Trump yuko tayari kuzungumza na maduro kuhusu magenge ya walanguzi Mexico
Ikulu ya Marekani imethibitisha kwamba nchi hiyo imetowa msaada wa kiintelijensia uliofanikisha operesheni hiyo ya kukamatwa El Mencho. Rais Claudia Sheinbaum ametowa wito wa utulivu nchini humo.