1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
UchumiUlaya

Mawaziri wa biashara wa Ulaya wakosoa ushuru wa Trump

15 Julai 2025

Mawaziri wa biashara wa nchi wanachama wa Umoja wa Ulaya kwa pamoja wamekosoa uamuzi wa Rais Donald Trump wa Marekani wa kutaka kuziwekea ushuru wa asilimia 30 bidhaa kutoka kanda hiyo.

Kamishna wa Biashara wa Umoja wa Ulaya Maros Sefcovic
Kamishna wa Biashara wa Umoja wa Ulaya Maros Sefcovic akizungumza na waandishi habari kabla ya kuanza mkutano wa mawaziri wa biashara wa kanda hiyo mjini Brussels.Picha: Yves Herman/REUTERS

Mawaziri hao waliokutana kwenye makao makuu ya Umoja wa Ulaya mjini Brussels, wamesema tangazo la Trump la kutaka kuweka kiwango hicho cha ushuru "halikubaliki"  na wameapa kuwa watachukua hatua za kujibu mapigo.

Mkutano wao umefanyika baada ya Trump kuelezea azma yake ya kuzitoza ushuru bidhaa kutoka mataifa ya Umoja wa Ulaya, uamuzi unaotishia kuwa na taathira kwa serikali, kampuni na walaji wa pande zote mbili. 

Trump alisema ushuru huo mpya utaanza kufanya kazi Agosti mosi kama hakutapatikana makubaliano baina ya pande hizo mbili.

Mawaziri hao wa biashara wamesema watafanya kazi pamoja kutafuta kataba wa biashara na Marekani au watachukua hatua za kujibu mapigo.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW