1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mawaziri wa EU na AU-wazingatia uamuzi wa mahakama Congo

Sekione Kitojo
22 Januari 2019

Umoja wa Ulaya na Umoja wa Afrika zimesema  kwamba zimezingatia uamuzi wa mahakama ya katiba ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya  Congo kumuunga mkono rais mteule Felix Tshisekedi, wakiashiria kwamba wanaweza kufanya nae kazi.

Federica Mogherini Hohe Vertreterin EU Aussenpolitik
Picha: Consilium/M. Salerno

Wakiulizwa  kuhusiana  na  uchaguzi  wa  hapo  Desemba  30, viongozi  wa  Umoja  wa  Ulaya  na  Umoja  wa  Afrika wamesema kwamba  wamejadiliana kuhusu  matokeo  ya   uchaguzi  huo  katika mkutano  wao  mjini  Brussels, wakidokeza  kuhusu  uungaji  mkono wa  mahakama   kwa  Tshisekedi. Maafisa hao  katika  mkutano  na waandishi  habari  hawakusema  wazi  hadharani  kwamba wanamtambua  Tshisekedi  kama  mshindi , na hata hawakumpongeza.

"Tumezingatia  tamko la  mahakama  ya  katiba, changamoto  ya rais  mpya  ni  kubwa  katika  masuala  mengi,"  mkuu  wa  sera  za mambo  ya  kigeni  wa Umoja  wa  ulaya  Federica Moghrini aliwaambia  waandishi  habari , akiwa  pamoja  na  wajumbe  wa Umoja  wa  Afrika.

"Tunafikiri  yote  haya  yanahitaji  kwamba  rais  ni  lazima  awe nguvu  ya  kuunganisha," Mogherini  amewaambia  waandishi habari, akisema  Umoja  wa  Ulaya  utaendelea  kufanyakazi  kwa karibu  na  Congo.

Rais mteule wa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo Felix TshisekediPicha: Reuters/O. Acland

Tukotayari kufanyakazi  na Congo

Waziri  wa  mambo  ya  kigeni  wa  Rwanda  Richard Sezibera, ambaye  anauwakilisha  Umoja  wa  Afrika  katika  mkutano  wa mawaziri  wa  mambo  ya  kigeni  wa  makundi  hayo  ya  mataifa , pia  amesema  amezingatia  uamuzi  huo  wa  mahakama.

"Umoja  wa  Afrika unatambua kwamba  taasisi  za  jamhuri  ya kidemokrasi  ya  Congo  zimetangaza  matokeo  ya  mwisho  na unaendelea  kuwa  na  dhamira ya  kufanyakazi  pamoja  na  watu wa  Congo  katika  kuendelea  kushughulikia changamoto  ambazo zimebakia."

Kamishna  wa  Umoja  wa  Afrika  anayehusika  na  masuala  ya amani  na  usalama Smail Chergui, ambaye  amezungumza  baada ya  Mogherini  na  Sezibera, amesema  yuko  tayari  kufanyakazi  na Tshisekedi   pamoja  na  vyama  vyote  vya  kisiasa  nchini  Congo lakini  alikata  kutoa  maelezo  zaidi.

Rais wa mahakama ya DRC Noel Funga (katikati) akiwaongoza majaji watano , akitoa taarifa mjini Kinshasa tarehe 15, Januari 2019.Picha: Getty Images/AFP/T. Karumba

Mahakama  ya  katiba  ya Congo  mapema  siku  ya  Jumapili ilikataa  malalamiko  ya  mshindi wa  pili  wa  uchaguzi  nchini  humo  Martin Fayulu  kwamba uchaguzi umetendewa  kinyume kwa  kuunga  mkono ushindi  wa Tshisekedi, na  upinzani  dhidi  ya  uchaguzi  huo  unaonekana kulainika.

Mwandishi: Sekione  Kitojo / rtre

Mhariri: Daniel Gakuba

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW