1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mawaziri EU wahadhari wito wa kususia mikutano ya Hungary

22 Julai 2024

Mawaziri wa mambo ya nje wa Umoja wa Ulaya wanaokutana mjini Brussels kujadili mizozo ya Ukraine na Gaza, wameeleza kukasirishwa na hatua ya waziri mkuu wa Hungary kufanya ziara Urusi.

Viongozi wa Umoja wa Ulaya wakiwa katika mkutano
Viongozi wa Umoja wa Ulaya wakiwa katika mkutanoPicha: Guido Bergmann/BPA/picture alliance

Mawaziri wa mambo ya nje wa Umoja wa Ulaya wanaokutana mjini Brussels, kujadili kuhusu mgogoro wa Ukraine na Mashariki ya Kati, wamezungumzia kwa tahadhari pendekezo la  kuususia mkutano ujao usiokuwa rasmi ulioandaliwa kufanyika mjini Budapest, Hungary.

Pendekezo hilo limetolewa kufuatia ghadhabu zilizoenea,Umoja wa Ulaya  dhidi ya waziri mkuu wa Hungary Viktor Orban  kutokana na hatua aliyoichukuwa hivi karibuni ya kufanya ziara kivyake,  mjini Moscow katika kile alichokiita ujumbe wa amani.

Soma pia:Mawaziri wa EU kukutana na kuijadili Ukraine na Gaza

Orban alimtembelea pia rais Xi Jinping mjini Beijing na mgombea urais wa Marekani wa chama cha Republican, Donald Trump.

Waziri wa mambo ya nje wa Ujerumani, Annalena Baerbockwakati akiwasili kwenye mkutano wa leo mjini Brussels amesema, ziara za siku chache za kiburi zilizofanywa na Orban zimesababisha hasira lakini mwenye maamuzi ya kutoa agizo la kuusisia mkutano wa Hungary ni Joseph Borrell ambaye ni mkuu wa sera za nje wa Umoja wa Ulaya.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW