1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaUrusi

Mawaziri wa EU waidhinisha vikwazo vipya dhidi ya Urusi

28 Mei 2024

Umoja wa Ulaya umewalenga majaji kadhaa wa Urusi na vikwazo vikali kupitia mfumo mpya wa vikwazo ulioidhinishwa jana kuadhibu ukiukaji mkubwa wa haki za binaadamu nchini Urusi.

Mkuu wa sera za kigeni wa Umoja wa Ulaya Josep Borrell
Mawaziri wa mambo ya nje wa Umoja wa Ulaya waliidhinisha mfumo mpya wa vikwazo kwa UrusiPicha: FRANCOIS WALSCHAERTS/AFP/Getty Images

Mfumo mpya wa vikwazo ulianzishwa kufuatia kifo cha kiongozi wa upinzani Urusi Alexei Navalny na unawalenga watu na mashirika yanayohusika na ukandamaziji wa upinzani. Jumla ya watu 19 nchini Urusi wamelengwa wakiwemo maafisa wa idara ya mahakama ya Urusi, waendesha mashitaka wa serikali na maafisa wa usalama waliohusika na kufungwa jela kwa Navalny.

Mkosoaji huyo wa serikali ya Urusi alifariki dunia katika mazingira ya kutatanisha akiwa katika jela ya eneo la Siberia mwezi Februari. Kifo chake kinatajwa na wengi kusababishwa na mazingira magumu mikononi mwa mamlaka za Urusi.

Soma pia: Urusi yakemea pendekezo la kutumia mapato ya mali zake zilizozuiwa

Maafisa wa Urusi waliohusika na kushtakiwa kwa mwanaharakati wa haki za binaadamu Oleg Orlov pia walijumusihwa. Bado hakuna makubaliano yaliyofikiwa kuhusu duru ya 14 ya vikwazo dhidi ya Urusi kwa vita vyake nchini Ukraine. Kwa mara ya kwanza, sekta ya gesi asilia ya Urusi yenye faida kubwa inazingatiwa.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW