Mawaziri wa G7 kujadiliana kuhusu Ukraine na Sudan Canada
12 Novemba 2025
Matangazo
Ripoti zinaarifu kuwa mbali na kutafuta njia ya kuumaliza mzozo huo uliodumu kwa miaka minne, huenda kukajadiliwa njia za kuyafadhili mahitaji ya Ukraine katika vita vyake na Urusi.
Mawaziri hao wanakutana wakati ambapo Rais wa marekani donald Trump aliziwekea vikwazo kampuni mbili kuu za mafuta za Urusi mwezi Oktoba akidai Rais Vladimir Putin hataki kuumaliza mzozo huo.
Waziri wa mambo ya kigeni wa Italia amesema kutakuwa pia na mazungumzo kuhusu vita vya Sudan ambavyo vimesababisha mzozo mkubwa zaidi wa kiutu duniani.