1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mawaziri wa G7 kujadiliana kuhusu Ukraine na Sudan Canada

12 Novemba 2025

Mawaziri wa nchi za kigeni wa mataifa saba yaliyoendelea kiviwanda duniani G7, wanakutana nchini Canada kwa mazungumzo yanayotarajiwa kujikita kwenye mzozo wa Ukraine.

Kanada Alberta 2025 | G7-Gipfel | Präsident Selenskyj trifft Premierminister Carney
Picha: Ukrainian Presidency/Anadolu/picture alliance

Ripoti zinaarifu kuwa mbali na kutafuta njia ya kuumaliza mzozo huo uliodumu kwa miaka minne, huenda kukajadiliwa njia za kuyafadhili mahitaji ya Ukraine katika vita vyake na Urusi.

Mawaziri hao wanakutana wakati ambapo Rais wa marekani donald Trump aliziwekea vikwazo kampuni mbili kuu za mafuta za Urusi mwezi Oktoba akidai Rais Vladimir Putin hataki kuumaliza mzozo huo.

Waziri wa mambo ya kigeni wa Italia amesema kutakuwa pia na mazungumzo kuhusu vita vya Sudan ambavyo vimesababisha mzozo mkubwa zaidi wa kiutu duniani.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW