1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaUkraine

Mawaziri wa kigeni wa EU waitembelea Bucha

31 Machi 2026

Mkuu wa Sera za Nje wa Umoja wa Ulaya, Kaja Kallas, anaongoza ujumbe wa mawaziri wa mambo ya kigeni wa Ujerumani, Poland na Italia kukitembelea kitongoji cha Bucha cha Ukraine kilichokombolewa kutoka jeshi la Urusi.

Kaja Kallas wa Umoja wa Ulaya
Mkuu wa Sera za Nje wa Umoja wa Ulaya, Kaja Kallas, anaongoza ujumbe wa mawaziri wa kigeni wa mataifa wanachama wa Umoja huo kukitembelea kitongoji cha Bucha nchini Ukraine siku ya Jumanne (Machi 31, 2026).Picha: John Thys/AFP

Ziara hiyo inakusudia kuadhimisha miaka minne tangu wilaya hiyo ya mji mkuu wa Ukraine, Kiev, kukombolewa kutoka mikononi mwa wanajeshi wa Urusi na kuibuwa ukatili mkubwa wa kivita uliotendeka.

Bucha, iliyo magharibi mwa Kiev, ilikaliwa na vikosi vya Urusi katika siku za mwanzo za vita vilivyoanzishwa na Urusi mnamo Februari 2022.

Baada ya wanajeshi wa Ukraine kufanikiwa kukirejesha mikononi mwao, miili ya raia ilikutikana imetapakaa kwenye mitaa ya kitongoji hicho, huku ikiwa imefungwa mikono kwa nyuma.

Haraka, Bucha ikageuka kuwa alama ya uhalifu wa vita hivyo, na baadaye Umoja wa Mataifa ulithibitisha vifo vya mamia ya raia.

Maafisa wa Urusi wanaendelea kukanusha tuhuma za mauaji hayo na badala yake wanadai ukatili wa Bucha lilikuwa tukio lililobuniwa na Ukraine yenyewe.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW