1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaJapan

Mawaziri wa mambo ya kigeni wa G7 kujadili usalama wa Ulaya

14 Aprili 2023

Mawaziri wa mambo ya kigeni wa kundi la mataifa tajiri la G7 watakutana mwishoni mwa juma mjini Tokyo kwa mazungumzo yatakayotuama juu ya usalama wa bara la Ulaya na kanda ya bahari ya Hindi na Pasifiki

Deutschland | G7 Außenministertreffen in Münster
Serikali za mataifa ya kundi la G7 zinaonyesha mshikamano na UkrainePicha: Wolfgang Rattay/AP Photo/picture alliance

Mkutano huo wa siku tatu utakaoanza mnamo Jumapili kwenye mji wa mapumziko wa Karuizawa unafanyika chini ya kiwingu cha vita kati Urusi na Ukraine na kuongezeka kwa kitisho cha China dhidi ya kisiwa cha Taiwan.

Soma pia: Wanadiplomasia wa G7 washikamana na Ukraine

Afisa mmoja wa wizara ýa mambo ya nchi za nje ya Japan amesema usalama wa Ulaya na kanda ya bahari ya Hindi na Pasifiki hauwezi kujadiliwa kwenye jukwaa tofauti kwa sababu yanafungamana.

Mkutano huo utakaowaleta pamoja mawaziri kutoka Marekani, Japan, Ujerumani, Uingereza, Ufaransa, Canada na Italia ni maandalizi ya mkutano wa kilele wa viongozi wakuu wa nchi za G7 utakafanyika Hkwenye mji wa Hiroshima mwezi ujao.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW