1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mawaziri wa kigeni wa UAE, Israel kufanya mazungumzo Berlin

Sekione Kitojo
6 Oktoba 2020

Mawaziri wa mambo ya kigeni wa  Israel na Umoja wa Falme za Kiarabu wametembelea kumbukumbu ya mauaji ya Wayahudi Holocaust  mjini Berlin kabla ya mkutano wao wa kwanza wa kihistoria katika mji huo mkuu wa Ujerumani.

Deutschland Israel Außenminister Heiko Maas  Gabi Ashkenazi
Waziri wa mambo ya kigeni wa Ujerumani Heiko Maas (Kulia) na mgeni wake Gabi Ashkenazi (kushoto)Picha: Reuters/M. Tantussi

Wakati  huo huo balozi wa  Ujerumani  nchini  Belarus  Manfred  Huterer, ameondoka  kwa  muda  nchini  humo, kwa  mujibu wa  vyanzo katika  ofisi  ya  wizara ya  mambo ya  kigeni  ya Ujerumani  kabla ya mkutano  wa  kansela  Angela  Merkel  na  kiongozi  wa  upinzani nchini  humo, Slevtlana  Tikhanovslaya. 

Waziri wa mambo ya kigeni wa UAE Abdullah Zayed al-Nahyan (kushoto) Picha: picture-alliance/dpa

Waziri wa  mambo  ya  kigeni  wa  Israel Gabi Ashkenazi  na mwenzake  wa  UAE Sheikh Abdullah bin Zayed al-Nahyan walisalimiana  kwa  kugusana  viwiko  vya  mkono  ikiwa  ni  hatua za  kujikinga  na  virusi  vya  corona, wakati  walipokutana  ana  kwa ana  kwa  mara  ya  kwanza  baada  ya  nchi  zao, ambazo  hapo zamani  zilikuwa  mahasimu  wakubwa, kutia  saini  makubaliano yaliyosimamiwa  na  Marekani  katikakti  ya  mwezi  Septemba kurejesha  uhusiano  wao  wa  kibalozi.

Wakiambatana  na  mwenyeji  wao, waziri wa  mambo  ya  kigeni  wa Ujerumani  Heiko Maas, mawaziri  hao  wawili  walitembea  katika eneo  hilo  la  kumbukumbu, lililo  la  matofali  makubwa  ya  saruji 2,700 yaliyowekwa   katika  eneo  ambalo  ni  sawa na  viwanja vitatu  vya  mpira.

Ni kumbukumbu  ya  Wayahudi milioni  sita  waliouwawa  na  utawala wa  kinazi  wa  Adolf Hitler.

Ziara  hiyo  ya  Sheikh Abdullah  katika  kumbukumbu  ya  Holocaust ni  hatua  ya  kiishara  tu,  ikionesha  kubadilka kwa  mtazamo  katika mataifa  ya  Kiarabu  kuelekea  Israel  na  wayahudi.

Kumbukumbu ya mauaji ya Wayahudi holocaust mjini Berlin Picha: Getty Images/S. Gallup

 

Mizozo ya  kisiasa  imesababisha  hali  mbaya  ya  wasi  wasi  kati ya  dini  ya Kiislam  na  ya Kiyahudi  pamoja  na  kukana  kutokea holocaust kitu  ambacho  kimekuwapo kwa  kiasi  kikubwa  katika mataifa  mengi  ya  Kiarabu.

Maas aliita  ziara  hiyo  kuwa  ni heshima  kubwa  ambayo   wizara za  mambo  ya  kigeni  ya  Israel  na  Emirati zimeipatia  Ujerumani kama  sehemu kwa  ajili  ya mkutano  wao  wa  kwanza  wa kihistoria.

Wakati  hayo  yakitokea  balozi  wa  Ujerumani  nchini  Belarus Manfred Huterer, ameondoka  kwa  muda  nchini  humo, kwa  mujibu wa  chanzo  katika  ofisi  ya  waziri  wa  mambo  ya  kigeni  ya Ujerumani  mjini  Berlin.

Huterer  aliondoka , "ili  kuongoza  majadiliano  mjini  Berlin"  kwa misingi  ya  mshikamano  na  Poland  na  Lithuania,  ofisi  hiyo imesema.

Maelezo ya kumbukumbu ya mauaji ya Wayahudi holocaust katikati ya mju mkuu wa Ujerumani Berlin.Picha: picture-alliance /dpa/U. Baumgarten

Poland na  Lithuania  zimewaita  nyumbani  mabalozi  wake  nchini Belarus  kwa  ajili  ya  mashauriano  kufuatia  madai  ya  Belarus kwamba  nchi  hizo zipunguze uwepo  wa  wanadiplomasia  wao nchini  humo, waziri  wa  mambo ya kigeni  wa  Lithuania  Linas Linkevicius  alisema  katika  taarifa  mapema  leo.

Kansela  wa  Ujerumani  Angela  Merkel  anatarajiwa  kukutana  na kiongozi  wa  upinzani wa  Belarus  anayeishi  uhamishoni Svetlana Tikhanovskaya  kwa  mazungumzo  mjini  Berlin  leo, wakati maandamano  makubwa  yanaendelea   nchini   Belarus  dhidi  ya rais Alexander Lukashenko  kurejea  madarakani.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW