1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mawaziri wa Nje wa NATO wakutana

3 Desemba 2009

Mawaziri wa mambo ya nje wa nchi za jumuiya ya kijeshi ya nato leo wanakutana mjini Brussels kuanza majadiliano ya siku mbili baada ya rais Barack Obama kutangaza mkakati mpya wa Afghanistan.

MontagePicha: AP/DW

Mawaziri  hao watajadili  hasa njia  za kuliimarisha  jeshi  la  kimataifa -ISAF nchini  Afghanistan na juu  ya kuwaingiza  wanachama wapya.

Katibu  mkuu   wa  mfungamano  wa kijeshi wa  nato Anders Fogh Rasmussen alisafiri sana  katika  wiki zilizopita.

Katibu Mkuu wa NATO l Anders Fogh RasmussenPicha: AP

Lengo la  ziara  alizofanya lilikuwa kuzishawishi  nchi wanachama wa  nato zitoe askari  zaidi ili kuliimarisha  jeshi la  kimataifa ,linaloongozwa na nato nchini  Afghanistan.

Kabla ya  kuanza mkutano  wa leo  wa mawaziri   wa mambo ya  nje  wa nchi za NATO mjini, Brussels katibu mkuu Rasmussen  alisisitiza   kwamba  vita vya  nchini   Afgnaistan  siyo  jukumu   la Marekani  pekee  yake.


´´Vita  hivi siyo vya  Marekani peke  yake. Yanayotokea  nchini  Afghanistan yanawahatarisha dhihiri wananchi  katika  nchi  zetu  zote"

Katibu mkuu huyo amesema  ni  kutokana  na  hatari  inayotokea Afghanistan kwamba ni lazima  kuliimarisha jeshi  la kimataifa linaoongozwa  na nato nchini  Afghanistan  ISAF kwa kuongeza  idadi  ya  askari.

Marekani  imeamua  kupeleka wanajeshi alfu  30 zaidi nchini Afghanistan  ili kuimarisha harakati za kupambana  na magaidi wa alkaida  na wapinzani  wa kitaliban.

Katibu  mkuu  wa  NATO  bwana  Rasmussen amesema amehakishiwa kupata  askarri alfu tano  zaidi  kutoka wanachama  wengine  wa  nato.

Kwa mujibu wa  duru za kidiplomasia, Georgia imeahidi kuongeza wanajeshi mia  770  na Uturuki imeahidi  askari  800 zaidi kwa  ajili   ya Afghanistan  na Poland  imethibitisha kwamba  itatoa  askari wengine  600.

UJERUMANI

Lakini Ujerumani  bado haijakuwa tayari kutekeleza maombi ya  kuongeza askari wake nchini  Afghanistan.

Waziri wa Nje wa Ujerumani Guido WesterwellePicha: AP

Waziri wa mambo ya nje  wa  Ujerumani Guido  Westerwelle ameeleza   kwa nini.

´´Kwanza inahusu malengo  na mikakati. Na ndipo baada ya hapo  vipatikane vifaa vya kutuwezesha  kufikia malengo  hayo .Mjadala uliopo nchini mwetu unaogusia tu suala la askari  wangapi wanaopaswa kupelekwa; mjadala kama huo tunaupinga."

Kwenye mkutano woa  wa leo mjini  Brussels mawaziri  wa   mambo  ya nje wa chi za nato pia  watajadii  suala la kuupanua mfungamano wao. Pamoja na  mengine  wataamua iwapo Montenegro  na  Bosnia Herzegovina zitaingizwa kwanza   katika hatua ya kwanza  ya kuelekea  kwenye uanachama.
Mwandishi /Birgit Schmeitner//ZA

Imetasfiriwa  na /Mtullya Abdu.

Mhariri/Hamidou Oummilkheir