1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mawaziri wa Ulinzi wa Urusi, Iran na Syria wakutana Moscow

24 Aprili 2023

Mawaziri wa Ulinzi na wakuu wa intelijensia kutoka Urusi, Iran, Uturuki na Syria watafanya mazungumzo, ikiwa ni ishara zaidi ya ushirikiano wa karibu kati ya Uturuki na Syria.

Russland Moskau | Türkischer Verteidigungsminister Hulusi Akar und der türkische Geheimdienstchef Hakan Fidan
Picha: DHA

Hayo yametangazwa leo na waziri wa Ulinzi wa Uturuki Hulusi Akar.

Akar amesema lengo la mazungumzo hayo yatakayofanyika Moscow kesho Jumanne, ni kusuluhisha matatizo ambayo yamesababishwa na vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini Syria na kupatikana kwa amani ya kanda hiyo.

Nchi zote zinazohudhuria mkutano huo zilihusika katika vita vya Syria, huku Urusi na Iran zikiunga mkono utawala wa rais Bashar al-Assad na Uturuki ikiwaunga mkono waasi kutoka kaskazini mwa Syria.

Mnamo mwezi Disemba, mawaziri wa ulinzi wa Syria, Urusi na Uturuki walikutana mwanzo ili kutuliza mvutano kati ya Damascus na Ankara.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW