1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mawaziri wa Israel wataka Ukingo wa Magharibi kunyakuliwa

21 Septemba 2025

Mawaziri wawili wa Israel walio na siasa kali za mrengo wa kulia wametoa wito wa kunyakuliwa kwa Ukingo wa Magharibi unaokaliwa na Israel kufuatia tangazo la Uingereza, Canada na Australia kulitambua taifa la Palestina.

Israel Jerusalem 2025 | Waziri Itamar Ben-Gvir mjini Jerusalem
Waziri mwenye siasa kali za mrengo wa kulia nchini Israel Itamar Ben Gvir,Picha: Ammar Awad/REUTERS

Mawaziri wawili wa Israel walio na siasa kali za mrengo wa kulia wametoa wito wa kunyakuliwa kwa Ukingo wa Magharibi unaokaliwa na Israel kufuatia tangazo la Uingereza, Canada na Australia kulitambua taifa la Palestina. Waziri wa usalama wa taifa Itamar Ben Gvir, amesema leo kwamba tangazo la Uingereza, Canada, na Australia kulitambua taifa la Palestina, linahitaji hatua za haraka za kukabiliana na hali hiyo. Miongoni mwa hatua za haraka alizopendekeza ni kupititishwa kwa mamlaka ya kujitawala huko Yudea na Samaria na kuvunjwa kabisa kwa Mamlaka ya Palestina. Waziri huyo anakusudia kuwasilisha pendekezo la kupitishwa mamlaka ya kujitawala katika mkutano ujao wa baraza la mawaziri. Naye waziri wa fedha Bezalel Smotrich, ambaye mara kadhaa ametaka Ukingo wa Magharibi kunyakuliwa, naye alitoa kauli kama hiyo.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW