1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaColombia

Colombia: Serikali yaanza mazungumzo ya amani na waasi

9 Oktoba 2023

Serikali ya Colombia na kundi lililogawanyika la shirika la zamani la waasi FARC zimeanza mazungumzo ya amani.

Rais wa Colombia Gustavo Petro
Rais wa Colombia Gustavo PetroPicha: Fernando Vergara/AP/picture alliance

Kulingana na Tume ya Juu ya Colombia, wapatanishi kutoka serikalini na wajumbe wa kundi la Estado Mayor Central (EMC) wanakutana kuanzia siku ya Jumapili katika manispaa ya Tibú karibu na mpaka wa Venezuela kwa ajili ya mazungumzo hayo ya amani.

Wajumbe wa pembeni kwenye mazungumzo hayo ni Umoja wa Mataifa Marekani, Kanisa Katoliki, Umoja wa Ulaya, Norway, Uswizi, Ireland na Venezuela.

Soma pia:Colombia yaongoza kwa mauaji ya wanaharakati wa mazingira

Rais wa Colombia Gustavo Petro amesema mazungumzo ya amani na kundi la waasi la mrengo wa kushoto la ELN pia yanaendelea na pia ameyaalika makundi mengine ya waasi na wanamgambo kushiriki kwenye katika mazungumzo hayo ya amani.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW