1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mazungumzo ya kusitisha mapigano Gaza kuanza tena wiki ijayo

25 Julai 2025

Shirika la habari la Al-Qahera lenye uhusiano na serikali ya Misri limesema vyanzo vilivyo karibu na serikali vimedokeza juu ya kuanza kwa mazungumzo ya amani ya Gaza wiki ijayo

Palästinensische Gebiete Gaza-Stadt 2025 | Mann trägt getötetes Kind nach israelischem Luftangriff
Mazungumzo ya kusitisha mapigano Gaza yanatarajiwa kuanza tena wiki ijayoPicha: Mahmoud Issa/REUTERS

Kuanza tena kwa mazungumzo hayo kunajiri baada ya Israel kupitia majibu ya wanamgambo wa Hamas.

Al-Qahera imesema Ujumbe wa Israel umeondoka siku moja baada ya Waziri Mkuu Benjamin Netanyahu kuiita nyumbani timu yake kwa mashauriano zaidi. 

Hamas: Ili kusitisha mapigano Israel ijiondoe Gaza

Mshirika mkuu wa Israel, Marekani pia nayo iliwaita nyumbani wajumbe wake kwa mashauriano jana alhamisi huku mjumbe wa Marekani kwaajili ya Mashariki ya Kati Trump Steve Witkoff akiishutumu Hamas kushindwa kuchukua hatua za kufanikisha mazungumzo hayo. 

Hamas imesema imeshitushwa na kauli ya Witkoff  ikisema msimamo wa kundi hilo umekaribishwa na wapatanishi na umefungua milango ya kufikia makubaliano. Pande zote mbili Israel na Hamas zinapitia shinikizo kubwa la ndani na nje ya maeneo yao ya kufikia makubaliano ya kusitisha vita hivyo vinavyokaribia mwaka wake wa pili. 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW