1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

MBS kufanya ziara Marekani Novemba 18

4 Novemba 2025

Marekani imesema kuwa Mwanamfalme wa Saudi Arabia Mohammed bin Salman atafanya ziara rasmi nchini humo tarehe 18 ya mwezi wa Novemba ambapo atafanya mazungumzo na Rais Donald Trump.

Saudi-Arabien Kronprinz Mohammed bin Salman
Picha: Leon Neal/Getty/AP/picture alliance

Ziara hiyo inakuja wakati ambapo Trump anaishinikiza Saudi Arabia kujiunga na orodha ya nchi ambazo zilitia saini mikataba wa Abraham, inayolenga kusawazisha mahusiano baina ya Israel na mataifa kadhaa ya Kiarabu.

Mwaka 2020 Trump alikubaliana na Umoja wa Falme za Kiarabu, Bahrain, Sudan na Morocco kusawazisha mahusiano yao na Israel.

Lakini Saudi Arabia qimesita kujiunga na orodha hiyo kutokana na kukosekana kwa hatua zitakazolifanya Palestina kuwa taifa huru.

Ila katika mahojiano Jumapili iliyopita, Trump alisema ana matumaini kuwa saudi Arabia itajiunga na mikataba hiyo.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW