1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
JamiiAlgeria

Meli iliyobeba tani 30,000 za mafuta yawasili Lebanon

28 Agosti 2024

Kaimu waziri wa nishati wa Lebanon Walid Fayad amesema meli ya Algeria inayobeba mafuta yanayohitajika kwa haraka imewasili nchini humo.

Libanon I Hafen von Beirut
Bandari ya Beirut na hifadhi yake ambayo kwa kiasi fulani iliharibiwa na mlipuko wa bandari wa mwaka 2020Picha: Joseph Eid/AFP/Getty Images

Meli hiyo iliyobeba tani 30,000 za mafuta imewasili kwenye pwani ya kituo cha mafuta cha Tripoli, kaskazini mwa Lebanon.

Meli hiyo imeelekezwa na kutia nanga karibu na matangi ya kuhifadhi mafuta, ikitoa zawadi kutoka kwa serikali ya Algeria kuisaidia Lebanon kuendesha mitambo yake ya umeme.

Soma pia: Lebanon inaadhimisha miaka 4 tangu mlipuko wa bandari huku hofu ya vita ikitanda

Waziri huyo wa nishati wa Lebanon ameonyesha matumaini kuwa mitambo mikuu ya umeme ya nchi hiyo itaanza kufanya kazi ifikapo kesho Alhamisi, na kwamba ugavi wa umeme unatarajiwa kuongezeka hadi saa nne hadi sita kwa siku.

Mtambo wa mwisho wa umeme uliokuwa unafanya kazi katika nchi hiyo iliyokumbwa na mgogoro, ulifungwa katikati ya mwezi Agosti kutokana na ukosefu wa mafuta.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW