1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Merkel ashikilia kuubadili mkataba wa Umoja wa Ulaya

Martin,Prema/ZPR18 Novemba 2011

Licha ya upinzani mkubwa kutoka Umoja wa Ulaya, Kansela wa Ujerumani Angela Merkel, anashikilia kuurekebisha Mkataba wa Umoja wa Ulaya, ili kuweza kuudhibiti mzozo wa madeni katika eneo la euro.

German Chancellor Angela Merkel speaks during a media conference at an EU summit in Brussels on Friday, March 25, 2011. EU leaders wrap up a two day summit on Friday focusing on the situation in Libya, the recent earthquake and tsunami in Japan, and new financial measures they hope will contain the debt crisis that has rocked the continent for more than a year. (Foto:Geert Vanden Wijngaert/AP/dapd)
Kansela Angela Merkel wa wa UjerumaniPicha: dapd

Kansela Merkel anazitaka nchi wanachama wa Umoja wa Ulaya, kukubali kuwa na viwango vya kukopa vinavyopaswa kuheshimiwa, kuziruhusu taasisi za umoja huo, kuingilia kati bajeti za taifa kwa kiwango fulani. Lengo ni kuwa na usimamizi bora wa kanuni za kusaidia kuleta utulivu wa sarafu ya euro.

Merkel amesema, nchi zinazokwenda kinyume na kanuni za mkataba wa Umoja wa Ulaya na kuhatarisha utulivu, zichukuliwe hatua.

Benki Kuu ya Ulaya isitumiwe kama chombo cha mwisho cha kusaidia katika mzozo wa madeni. Amesema, wanasiasa wanakosea kama wanaamini kuwa benki hiyo inaweza kusuluhisha tatizo la sarafu ya Euro iliyodhoofika.

Waziri Mkuu wa Uingereza, David CameronPicha: dapd

Leo Kansela Merkel anakutana na Waziri Mkuu wa Uingereza David Cameron mjini Berlin, kujadili hatua za kuchukuliwa kuhusiana na mzozo wa fedha.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW