1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Merkel ziarani barani Afrika

14 Julai 2011

Kansela wa Ujerumani, Angela Merkel amewasili Nigeria, kituo cha mwisho cha ziara yake barani Afrika.

Kansela wa Ujerumani, Angela MerkelPicha: piture-alliance/dpa

Leo Merkel, anatazamiwa kukutana na Rais wa Nigeria Goodluck Jonathan. Nigeria iliyo na idadi kubwa kabisa ya watu barani Afrika, ni mzalishaji mkubwa wa nane wa mafuta kote duniani, lakini nchi hiyo ina upungufu mkubwa wa umeme.

Wakati wa ziara hiyo nchini Nigeria, Merkel anatazamiwa kuunga mkono ushirikiano katika sekta ya nishati na malighafi, kama alivyofanya wakati wa ziara yake nchini Angola, kituo cha pili cha ziara yake barani Afrika. Alipokuwa Angola, aliunga mkono kuimarisha uhusiano wa kisiasa na kiuchumi kati ya Ujerumani na Angola. Alisema kuwa Ujerumani, ingependa kuwekeza katika sekta za miundo mbinu, viwanda na elimu.

Kansela Merkel(kulia) na Rais wa Angola Jose Eduardo dos SantosPicha: dapd

Vile vile Ujerumani ingeweza kushirikiana kutafuta mali ghafi zaidi nchini humo. Merkel alitamka hayo baada ya kukutana na Rais wa Angola José Eduardo dos Santos katika mji mkuu wa Angola, Luanda. Merkel alieanzia ziara yake nchini Kenya, amefuatana na Waziri wa Kilimo, Ilse Aigner na ujumbe wa wafanyabiashara.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW