Merz achaguliwa tena kwama mwenyekiti wa chama cha CDU
21 Februari 2026
Matangazo
Merz aliungwa mkono na asilimia 91.7 za kura za wajumbe 878 kati ya 963 zilizopigwa kwenye mkutano mkuu wa chama hicho huko Stuttgart.
Haya yalikuwa matokeo yake ya pili bora. Mnamo mwaka 2022, alichaguliwa kwa 94.6% ya kura kwenye mkutano wa chama hicho ulioandaliwa kwa njia ya video na baadaye kuthibitishwa kwa asilimia 95.3 ya kura kwa njia ya posta. Mwaka 2024, alipata 89.8% ya kura.
Baada ya kura hiyo, Merz aliwashukuru wajumbe hao na kuahidi ushirikiano bora zaidi ndani ya chama hicho.
Mkutano huo wa siku mbili umefanyika mwanzoni mwa mwaka wa uchaguzi wenye shughuli nyingi kwa CDU, huku chaguzi tano za majimbo zikitarajiwa kufanyika, mwezi Machi na Septemba, hali ambayo huenda ilichangia chama hicho kumuunga mkono Merz.