1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
UchumiChina

Merz aenda China kufanya mazungumzo na Rais Xi

24 Februari 2026

Kansela wa Ujerumani Friedrich Merz ametolewa wito na viongozi wa biashara kusisitiza ushindani wa haki na China anapojiandaa kwa mazungumzo na Rais Xi Jinping kesho Jumatano.

Ujerumani Berlin 2026 | Friedrich Merz akizungumza katika ufunguzi wa "Cafe Kyiv" ya Wakfu wa Konrad Adenauer
Kansela wa Ujerumani Friedrich Merz anakwenda China kwa mazungumzo na Rais wa China Xi Jinping kuhusu masuala mbalimbali Picha: Markus Lenhardt/dpa/picture alliance

Shirikisho la Viwanda vya Ujerumani (BDI) kupitia mjumbe wake Wolfgang Niedermark limemtaka Merz "kushughulikia waziwazi masuala kama vile uwezo kupita kiasi, upotoshaji kwenye ushindani na udhibiti wa mauzo ya nje ya malighafi muhimu.

Ametahadharisha ikiwa hakutakuwa na mabadiliko ya mwelekeo kwa upande wa China, ni wazi kutaibuka migogoro mipya ya kibiashara na Umoja wa Ulaya.

Merz anaondoka Jumatatu kwenda China kwa ziara yake ya kwanza tangu alipokuwa kansela mwaka uliopita na anatarajiwa kujadiliana na Xi masuala kuanza ushirikiano wa kiuchumi hadi ya usalama kama vita vya nchini Ukraine.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW