1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Merz awania kuchaguliwa tena kama mwenyekiti wa CDU

20 Februari 2026

Kansela wa Ujerumani Friedrich Merz anawania kuchaguliwa tena kuwa mwenyekiti wa chama cha kihafidhina cha Christian Democratic Union (CDU) katika mkutano mkuu wa chama hicho utakaofanyika mjini Stuttgart .

Deutschland Stuttgart 2026 | CDU-Parteitag | Bundeskanzler Friedrich Merz besichtigt Messehalle
Picha: Chris Emil Janßen/IMAGO

Merz anasaka uungwaji mkono mkubwa kutoka kwa wajumbe wa chama hicho kwa mara ya kwanza tangu kuwa kansela mnamo mwezi Mei mwaka 2025.

Wajumbe pia wataipigia kura hoja kutoka kwa kamati kuu ya utendaji, ambayo CDU inataka kutetea mabadiliko mapya katika soko la nyumba.

Kansela wa zamani, Angela Merkel, pia anatarajiwa kuhudhuria kongamano hilo la siku mbili kama mgeni rasmi, hii ikiwa ni mara yake ya kwanza kushiriki mkutano wa chama cha CDU tangu alipoondoka madarakani mwaka 2021.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW