1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Merz: Hakuna mpango unaoeleweka wa kumaliza vita Iran

10 Machi 2026

Kansela wa Ujerumani Friedrich Merz ameelezea wasiwasi wake leo juu kile alichosema kuwa ni kukosekana mpango wa pamoja kati ya Marekani na Israel wa kuvimaliza vita dhidi ya Iran.

Marekani Washington 2026 | Kansela wa Ujerumani Friedrich Merz
Kansela wa Ujerumani Friedrich Merz.Picha: Kay Nietfeld/dpa/picture alliance

Akizungumza mjini Berlin akiwa pamoja na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Czech Andrej Babis, Merz amesema kadri siku zinavyosonga mbele inaonesha kuna hatari ya mzozo huo kutanuka na hakuna mpango unaoeleweka wa kuumaliza.

Kiongozi huyo amesema ijapokuwa Ulaya inao mtizamo wa pamoja na Marekani na Israel linapohusika suala la Iran, lakini bara hilo haliko tayari kushuhudia vita visivyo na ukomo.

Pia amesema Ujerumani haitamani kuona Iran inasambaratika na kuzusha taathira mfano wa zile zilizoshuhudiwa baada ya vita vya Libya, Iraq na nchi nyingine kwenye kanda hiyo.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW