1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaUfaransa

MFS: Ufaransa na Italia huwanyanyasa wahamia

4 Agosti 2023

Shirika la Madaktari Wasio Mipaka (MSF) limesema kuwa wahamiaji wanaojaribu kutoka Italia kuingia Ufaransa kwenye mpaka wa Ventimiglia.

Symbolbild Migration
Picha: SAMEER AL-DOUMY/AFP/Getty Images

Kwenye Pwani ya Mediterania wanakabiliana na mateso makubwa kutoka kwa polisi wa Ufaransa huku Italia ikiwapa msaada hafifu na kukosa huduma muhimu.

MSF imesema Ufaransa imekuwa ikiwarejesha moja kwa moja nchini Italia wahamiaji wote wanaoingia nchini humo kinyume cha sheria, na mara nyingi hutumia mabavu, unyanyasaji na kuwazuia watu kiholela. Serikali ya Paris na Rome zote hazijatoa maoni kuhusu ripoti hiyo.

Kwa muda mrefu, suala la uhamiaji limekuwa kiini cha msuguano katika mahusiano kati ya Ufaransa na Italia huku kukiwa na mvutano ndani ya Umoja wa Ulaya kuhusu sera inayofaa ili kushughulikia vitendo vinavyoongezeka vya wahamiaji wanaotaka kuingia Ulaya hasa wakitokea Afrika Kaskazini.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW