1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

EURO 2024: Uswisi wafuzu baada ya kutoka sare na Ujerumani

24 Juni 2024

Katika mechi za Kombe la EURO 2024, jana usiku Ujerumani ambao wameshafuzu hatua ya mtoano, walilazimishwa sare ya 1-1 na Uswisi ambao pia matokeo hayo yamewawezesha kusonga mbele.

Euro 2024 Ujerumani yalazimishwa sare ya 1-1 na Uswisi
Mchezaji wa Ujerumani Jamal Musiala (kushoto) akijaribu kudhibiti mpira na kumzuia mchezaji wa Uswisi Remo Freuler wakati wa mechi yao mjini Frankfurt: 23.06.2024Picha: Michael Probst/AP Photo/picture alliance

Katika mechi nyingine, Hungary waliicharaza Scotland katika dakika za nyongeza bao 1-0. Wakiwa na pointi tatu na tofauti ya mabao, Hungary sasa watalazimika kusubiri ili kujua iwapo watafika hatua ya mtoano.

Soma pia: Shirika la reli la Ujerumani linanufaika kwa ongezeka la abiria katika kipindi hiki cha Euro 2024

Leo Jumatatu, Albania watashuka dimbani na Uhispania, huku Croatia wakimenyana na Italia.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW