1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaSudan

Miripuko na majibizano ya risasi vyasikika tena Khartoum

22 Mei 2023

Mashambulizi ya majibizano ya risasi pamoja na miripuko vimesikika tena katika mji mkuu wa Sudan Khartoum saa chache kabla ya muda wa kuanza utekelezwaji wa makubaliano ya kusitisha vita kwa wiki moja

FILE PHOTO: Sudan Karthoum
Picha: MOHAMED NURELDIN ABDALLAH/REUTERS

Makubaliano hayo ya usitishwaji mapigano yalifikiwa mwishoni mwa wiki huko Jeddah nchini Saudi Arabia. Jana Marekani na Saudi Arabia zilitangaza kwamba makubaliano ya kusitisha vita kati ya kambi mbili zinazopigana nchini Sudan yataanza usiku wa leo, kutoa nafasi kwa msaada wa kibinadamu kuwafikia raia wa Sudan.

Pande zote mbili kwenye mgogoro zilithibitisha kwamba zitaheshimu makubaliano hayo yaliyopongezwa pia na Umoja wa Mataifa, Umoja wa Afrika na Jumuiya ya maendeleo ya ushirikiano wa nchi za Mashariki mwa Afrika, IGAD.

Soma pia: Pande mbili hasimu zakubaliana kusitisha mapigano kwa wiki moja Sudan

Mpaka sasa kiasi watu 1,000 wameuwawa na zaidi ya milioni 1 wameachwa bila makaazi kufuatia mapigano ya zaidi ya wiki tano,yaliyoitumbukiza kwenye janga la kibinadamu nchi hiyo.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW